Mungu mkuu wa mipango



Download 1,15 Mb.
bet1/13
Sana24.06.2017
Hajmi1,15 Mb.
#14917
  1   2   3   4   5   6   7   8   9   ...   13
YOSHUA KWA MATAIFA.

Niombe nami nitakupa mataifa Zaburi 2:8

Maana na mipango.

MUNGU MKUU WA MIPANGO.

Yaandike maono haya. Yaandike wazi juu ya vibao, anayepita hapa apate kuyasoma.Hab 2:2



Maono: Sote tunayo maono, lakini si wote wanaojua namna ya kufikia na kutimiza maono ambayo Mungu ametuitia kuyatimiza. Mipango, misingi, wimarishaji, kufundisha na kuendeleza yote haya ni muhimu katika kuona kwamba maono yamekamilika. Imeshasemwa, toa dollar kwa mpango lakini dollar million kwa mwenye kufanyiza mpango kazi. Mungu ana mpango na pia anafanyiza kazi katika kila moja wetu na kupitia kwetu.

Mpango wa Mungu hudumu milele. Maazimio yake yadumu vizazi vyote. Heri taifa ambalo Mungu wake ni mwenyezi Mungu: Heri wale aliowachagua kuwa watu wake mwenyewe! Zab 33:11-12

Sisi sote tuna asili ya maono na mipango. Ila hatutambui asili hii. Kwa mfano tunaweza kuona kwa maono tukinunua matunda maana tuna njaa. Basi katika asili tunaanza kufikiri kuhusu na kupanga jinsi tutakavyoenda kununua. Tunapitia hali hii kila siku na mara nyingi kwa njia tofauti kwa siku. Haijalishi kama una cheo katika benki ya dunia, mzazi tu wa kawaida, huu ni ukweli katika maisha ya mwanadamu. Yoshua kwa mataifa wanaamini na kuimarisha na kufundisha watu wa Mungu msingi na thibitisho ya mtindo ya kuwezesha kufika maono ya Mungu maishani. Hivyo basi mpango mahususi ni nini? Mpango mahususi ni vile unavyojitahidi katika kuyafikia mambo yako ya sasa na usoni. Mpango mahususi huambatana na maswali manne ya muhimu.

Umekuwa wapi?

Uko wapi?

Unaelekea wapi?

Utafikaje kule unakoenda?

Mungu amedhibitisha mpango wa mahasusi jinsi ya kuuliza kazi ya msamaha kupitia kwa kristo na maandiko yake matakatifu ya kutuelezea chanzo chetu pahali tumekuwa, mahali tuko sasa ,kule tunaelekea na jinsi ya kufika pale. Tukitazama mfano wa Mungu kama mtindo wa maisha yetu, wacha tutazame mpango wake mkuu.



Maono

Kurejesha mshirika na mwanadamu.



Kazi au utume

Kuelezea haja ya msamaha wa dhambi kupitia damu ya Kristo Yesu.



Madhumuni au makusudio

Kuunganisha ulimwengu kwake.

Kumshinda adui.

Kuidumisha sheria ya Kristo duniani.



Hila au mikakati.

Kuita na kufanya agano na wateule wake.

Kuimarisha lengo la mpango wa kuufikia ulimwengu na taifa la Israeli.

Kupeana mwelekezo wa dhabihu hadi messia aje, kuutoa muda ufaao kupitia sheria zilizotengwa na bwana.

Kutuma majumbe maalumu wa kuendea na kuendeleza njia ya mwokozi.

Mbinu au mahiri.

Kuanzisha agano au kuweka, kubadilisha mtindo wa dhabihu, mahali na wakati.

Kuhitaji uwafibikaji, kufuata na kulinda na kuweka mpango.

Kufanya yote yanayotakikana.



Kuangalia na hatua zinazofuata.

Je Mungu alirejesha ushirika na mwanadamu?

Amefanya njia ya ukombozi?

Ulimwengu unaunganishwa kwake?

Sheria ya Kristo imeimarishwa duniani?

Hali ya mfano au kielelezo kama hii yaweza kuonekana katika maandiko (kwa mfano:kutaka kujenga banda au hema nyikani, kuingia kwenye mji wa ahadi, kujenga hekalu katika mji wa Yerusalemu na hata wewe).

Ratiba huenda na kuendea kuhusu mpango wake Mungu kwa kufika kilele cha maono yake ambaye Yesu mwenyewe alitufundisha.

“Kwa maana, ni nani miongoni mwenu ambaye akitaka kujenga mnara hataketi kwanza akadiria gharama zake ili ajue kama ana kiasi cha kutosha cha kuweka msingi na kushindwa kumaliza, watu watamcheka wakisema: ‘mtu huyu alianza kujenga,lakini hakumaliza. Luka 14:28-31



Yoshua kwa mataifa wamejitokeza katika hali ya kuonyesha hila ya mipango ,kuanzisha, kufundisha na makadirio ya kifedha kwa kila mmoja wao.Katika chuo cha Bibilia, kundi linalosimamia taifa au ulimwengu sote tumejitolea katika hila hii.

Hila ya Yoshua kwa mataifa.

Maono

Kazi

Madhumuni

Hila/ Mikakati

Mbinu

Hatua zinazofuata

Kufundisha mataifa.

Wasio amini kuamini.

Kuanzisha vituo vya kufundisha bibilia.

Ufundishaji.

Kuinua.

Kuangalia na kuona matokeo kuhusiana na kiulindaji.




Maani kuwa wanafunzi.

Kufundisha.

Uongozi.

Kusajili.







Wanafunzi kuwa viongozi.

Kuimarisha.

Uwajibikaji.

Kupanga na kusimamia.







Viongozi kuwa baba.

Kuzalisha.




Usimamizi wa fedha.







Baba kuwa kiongozi wa viongozi.

Kutia moyo.
















Kukomboa.
















Kupeana.
















Kufanya ieleweke.
















Kufanyika kuwa.











MAJUKUMU YA ZIADA


Kundi la viongozi katika dunia

Kustawisha kila taifa kati ya bara zote:Amerika, Uropa,Uesia, Urusi,Mashariki ya kati na Kusini mwa visiwa vya Pasifiki.

Kufanya kazi katika kushirikiana na mkurugenzi wa ulimwengu na mataifa yote.




Kuomba fedha zitakazo saidia maeneo haya katika hali ya kibinadamu, ujenzi na elimu.

Kumalizia ripoti za maendeleo katika bara zote.







Kupeana vyeti.



Kundi la viongozi wa taifa

Kuimarisha na kuangalia vikundu vya mataifa na eneo ndogo.




Kuimarisha miundomsingi.




Kufanya kazi kushirikiana na viongozi wa kimataifa na eneo ndogo.

Kukamilisha ripoti ya maendeleo katika taifa.

Kupeana vyeti.



Kundi la viongozi katika eneo ndogo.

Kuanzisha au kupanda, kuimarisha na kuangalia chuo cha bibilia.




Kufanya kazi kwa kushirikiana na viongozi wa kitaifa pamoja na vyuo vingine.




Kukamilisha ripoti ya maeneo madogo.




Kupeana vyeti.


MAONO.

Maono ni nini?

Maono inajumulisha uwazi wa hali au mfano kuu. Yanadhihirisha hitaji kuu la mtu au kusanyiko wanalohitaji kulifikia, ni mfano wa picha ya usoni iletayo juhudi maishani mwa mtu.



Maono ya Yoshua kwa mataifa: Kufundisha mataifa.

“Yesu akaja karibu akawaambia,”Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.Nendeni basi, mkawafanye watu wa mataifa yote wawe wanafunzi wangu.

Mkibatiza kwa jina la baba na la mwana na la roho mtakatifu. Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni. Nami nipo pamoja nanyi siku zote ,na mpaka mwisho wa nyakati zote. Mathayo 28:18-20.

Yoshua kwa mataifa wamejitokeza kufundisha viongozi kuzaa na kupeana maono katika uwezo wao. Neno la sema wazi, pasipo na maono watu huangamia. Watu wamungu wanategemea maono, nayo maono yako juu ya watu wa mungu. Pasipo na maono watu huangamia, na pasipo kuweko watu maono yaangamia. Moja bila mwingine hawezi kuendelea kuzalisha au la muhimu sana pinga maovu katika ulimwengu.



Kazi.

Ni nini hali ya utendaji kazi?

Hali ya utendaji kazi inadhihirisha lengo na jinsi unavyo fikia maono yako. Yapaswa kuwa fupi, inayolenga, rahisi kueleweka na kijana na inayo weza kukaririwa.



Ni nini hali ya utendaji kazi ya Yoshua kwa mataifa?

  • Wasioamini kufanyika waamini.

  • Waamini kufanyika wanafunzi.

  • Wanafunzi kufanyika viongozi.

  • Viongozi kufanyika baba.

  • Baba kufanyika kiongozi wa viongozi.


Madhumuni.

Madhumuni ni nini?

Madhumuni huweka alama kwa matokeo yanayotarajiwa kwa kutimiza maono. Maono yetu hutuvuta na kutupeleka katika maisha au mambo yajayo.



Madhumuni ya Yoshua kwa mataifa ni yapi?

Kuanzisha vituo vya vyuo vya bibilia kote duniani.

Kuyafundisha mataifa.

“Nendeni basi, mkawafanye watu wa mataifa yote wawe wanafunzi wangu, mkiwabatiza kwa jina la baba na la mwana na la roho mtakatifu. Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni. Nami nipo pamoja nanyi siku zote; Naam, mpaka mwisho wa nyakati.



Kuandaa kila mwanafunzi.

“Ndiye aliyewapa watu zaidi; wengine aliwajalia wawe mitume, wengine manabii, wengine wawe waenezaji injili, wengine wachungaji na walimu. Alifanya hivyo apate kuwatayarisha watu wote wa mungu kwa ajili ya kazi ya huduma ya kikristo ili kujenga mwili wa kristo na hivyo sote tufikie umoja wa imani na kumjua mwana wa mungu; tuwe watu waliokomaa na kuufikia utimilifu wake kristo mwenyewe. Basi hatutakuwa tena watoto, tukitupwa na kupeperushwa huko na huku kwa kila upepo wa mafundisho wanayozua watu wadanganyifu ili wawapotoshe wengine kwa hila kama tukiuzingatia ukweli kwa moyo wa mapendo tutazidi katika kila jambo kulingana na kristo ambaye ndiye kichwa, chini ya uongozi wake, viungo vyote vya mwili hushikamana pamoja na mwili hutegemezwa kwa msaada wa viungo vyake. Basi kila kiungo kikitekeleza kazi yake ipasavyo, mwili wote hukua na kujijenga katika upendo. (Waefeso 4:11-16)

Kazi yetu ni kuinua watu wahisi kuwa wenye afya zaidi, kukuwa na kufanikiwa, kuwa tofauti na wakudhani kuyafikia mambo yenye hawakudhani kuyafikia.

Kujizalisha kwa wengine.

Kuwa na tunda, matunda mengi na mengi zaidi na yatakayo dumu.(John 15)



Kukomboa watu wa mataifa.

“Kutokana na wazawa wako mataifa yote duniani yatabarikiwa kwa sababu wewe umeitii amri yangu (Mwanzo 22:18-19) kukomboa na kuvulia watu walimwengu wanaowakilishwa na jamii, elimu, serikali, soko, kuigiza na michezo.



Kuimiza kubadilisha kwa maisha kwa neno.

Kuhudumu na kuisi kupanuliwa kwa ufalme wanaposhuhudia.”Sasa ufalme wa ulimwengu ni wa Bwana wetu na Kristo wake.” (Ufunuo 11:15)



Kupeana nguvu zaidi za kufanya kazi katika mwili wa Kristo.

“Hapo akawaambia wanafunzi wake, mavuno ni mengi wafanyikazi ni wachache. Basi mwombeni mwenye mavuno atume wafanyikazi wavune mavuno yake. (Mathayo 9:37-38)



Kufafanua roho wa uwazi

“Basi, sisi tulio na hazina tuko tu kama vyombo vya udongo, ili ionekane wazi kwamba nguvu hiyo kuu yatoka kwa Mungu wala si kwetu sisi wenyewe.(2Wakorintho 4:7)

“Katika nyumba kubwa kuna bakuli na vyombo vya kila namna vingine ni vya fedha na dhahabu, vingine ni vya ubao na udongo,vingine vya matumizi ya heshima na vingine kwa ajili ya matumizi ya kawaida. Basi kama mtu atajitenga na kujitakasa mbali na mambo hayo yote maovu, atakuwa chombo cha matumizi ya pekee kwa sababu amewekwa wakfu, anamfaa bwana wake na yupo tayari kwa kila kazi njema.(2Timothy 2:20-21)

“Kwa sababu ana roho njema, maarifa, ujuzi wa kutafsiri ndoto, kufumbua fumbo na kutatua matatizo. Jina la mtu huyo ni Danieli.(Danieli 5:12)



Kufanyika kwa kujitegemea kifedha

Moja wapo ya mtazamo wetu ni kuyawezesha mataifa yawe ya kujimudu kifedha na pia kutoa kwa ajili ya mavuno kuu.


MIKAKATI.

Mikakati ni nini?

Mikakati ni hali ya kuleta pamoja mipango, hali na mambo yote yanayofanya kazi kati ya nadhiri yako na msimamo wa imani kukamilisha lengo.

Ama ni hali ya mpangilio wako mzuri, mambo mazuri unayoyafikiria sasa kwa ajili ya siku zijazo. Mikakati hii huhusu mambo ya muda mfupi na muda mrefu. Hivyo basi hali ya kuwa tayari kwa kubadilisha na kurekebisha ni muhimu unapo weka na kupanga mipango yako. Mpango mahususi lazima uwe na msingi kulingana na kanuni zake. (Katika nadhira na imani) Pia kuwa tayari kubadili na kurekebisha katika mipango zako.

Hali hii ya Mikakati hujumlisha mambo ma nne.

Umekuwa wapi?

Uko wapi sasa?

Unaelekea wapi?

Nani kwa njia gani utafika pale.

Je mikakati ya Yoshua kwa mataifa ni gani?

Yoshua kwa mataifa wana mambo matatu ambayo ni kufundisha, kuongoza na usimamizi.



Kufundisha.

Yesu akaja na kuwaambia : Nendeni basi mkawafanye watu wa mataifa yote kuwa wanafunzi wangu.

(mathayo 28:19)

Kuna njia moja yenye ukuu na uwezo zaidi ya kufundisha ulimwengu au mataifa. Mtu mmoja kwa wakati, kuwa naye ana kwa ana. Yesu kristo alikuwa na wanafunzi wake. Alikula nao, kutembea, kufundisha, kuhudumu, kurekebisha, kucheka na kulia pamoja nao. Wakati wake wa kipekee na karibu kwa wanafunzi wake, ulimpa fursa nzuri ya kuwaandaa na kuwatayarisha. Tumeitwa kwa mtindo huu wa mmoja kwa mwingine kama vile imesimuliwa na mtume Paulo katika(waefeso 4:11)



Ndiye aliye wapa watu zaidi, wengine aliwajali a wawa mitume, wengine manabii, wengine wainjilisiti na wengine wachungani na walimu kwa ajili ya kuwatayarishia watakatifu kwa sababu ya kazi ya huduma. Kwa kujenga mwili wa kristo, ili sote tuitikie utimilifu wa imani na ufahamu wa mwana wa mungu tuwe wa komavu na kuufikia utimilifu na ukamilifu wa kristo.

Tunatazamia mambo manne ya muhimu tunapo fundisha na kuandaa wanafunzi.

Kuwasaidia kuwa na ubora wa mwili, nafsi na roho.

Kuwasaidia kutambua utendaji wao na vipawa vyao katika mwili wa kristo na zaidi kuwahimiza jinsi ya kufanya huduma ya vijana, watoto na watu wazima.

Kuwasaidia kurekebisha na kufahamu mapenzi ya mungu.

Kuwasaidia kufikia utimilifu na kufaulu katika kazi ya huduma kwa njia ya mifano na ujuzi .

Kusaidia waumini na viongozi ili watazamie katika kristo.

Uongozi.

Yoshua kwa mataifa wamejitokeza kwa kuongoza watu moja wapo na msingi unao patikana rahisi na wa ukweli kwa wakati tuliomo, umenakiliwa na Stephene Corey.

Unasimamia vitu lakini unaongoza watu. Uongozi ni hali ya kuvutia! Kunao viongozi wazuri na viongozi wabaya. Kunao wale wanaovutia kwa uzuri na ubaya. Swali ni moja. Je sisi tu viongozi wa aina gani? Cheo hakileti tabia ila tu ubaya na uzuri ni kawaida. Ni hali ya kukubaliana inayosababisha uongozi wa kuwajibika katika maisha yetu. Hivyo basi yatupasa kuwa kujitolea kwa ukamilifu ambayo italeta kuaminika na tumaini na kuvutia kwa haki kizazi cha sasa na pia vizazi vijavyo.

Uongozi unahitaji kuwajibika ili kubadilisha maisha ya wafuasi kwa malezi, mafundisho. Viongozi wa kuzaliwa na viongozi wa kuandaliwa. Mfano ni Daudi (Kiongozi wa kuzaliwa.) Gidioni kiongozi wa kuandaliwa. Hata hivyo iwe wa kuandaliwa ni kuzaliwa au kuandaliwa. Sote tumeumbwa kwa mikono yake mungu kuongoza katika uwezo wetu wa kuvutia na kuendeleza ufalme wake mungu. Moyo wake mungu hautatosheleza mpaka sote tuwe viongozi kwa hali ya kipekee ya mwito wetu.

“Lakini nyinyi ni ukoo mteule, makuhani wa mfalme, taifa takatifu, watu wake mungu mwenyewe, mlio teuliwa kutangaza matendo makuu ya mungu aliyewaiteni kutoka gizani, akawaingiza katika mwanga wake mkuu. Wakati mmoja nyinyi hamkuwa watu wa mungu. Lakini sasa nyinyi ni watu wa wakati mmoja hamkupewa huruma ya mungu lakini sasa mmepokea huruma(1petro 2:9-10)

“Daudi akawafunza kwa moyo wake wote, akawaongoza kwa uhodari mkubwa. (Zaburi 78:72)

Tambua mtindo huu wa pekee uliopewa Musa.Basi Yethero akamwambia Musa Unavyofanya si vizuri utajidhuru mwenyewe na hawa watu kwa uchovu kwani hii ni kazi ngumu usiyowea kufanya pekee yako. Sikiliza shauri langu kwako na mungu awe pamoja nawe. Wewe utawakilisha watu mbele ya Mungu na kumletea mungu matatizo yao. Hali kadhalika utawafundisha amri na maamuzi ya mungu na kuwaonyesha jinsi inavyo wapasa kuishi na kufanya.Lakini kuhusu mambo mengine, chagua miongoni mwa watu;watu wanaostahili,watu wanao mcha Mungu, Waaminifu na wanaochukia kufungwa wapewe hao mamlaka wawe na jukumu la kuwasimamia watu katika makundi ya watu elfu, mia, hamsini, na kumikumi. Hao ndio watakao kuwa na vikao kila siku kutatua matatizo ya watu, matatizo magumu watakuletea wewe, lakini yale madogo madogo watayaamua wenyewe. Kwa njia hiyo kazi yako itarahisiswa maana watashirikiana nawe kwa juma hilo, ukifanya hivyo na kama ndivyo atakavyo Mungu. Utaweza kustahimili na watu hawa wote wataweza kurudi kwao kwa amani. (Kutoka 18:17-23)

Ni nani anayestahili kuchagua viongozi?

Kuwa na uwezo wa kutumika kwa kushirikiana na kuajibika.

Kuwa na hali ya kumcha Bwana.

Mtu wa kupenda ukweli.

Mtu asiyetamani.

Je hawa viongozi watafanya nini?

Kupeana mamlaka.

Hauwezi kuwa kiongozi mzuri kama haujui namna ya kupeana mamlaka. Kumbuka lengo letu ni kuwafanya wengine viongozi wakuu. Peana mamlaka kulingana na uwezo wa kiongozi jinsi awezavyo kuongoza. 10, 50, 100, 1000.



Kuwa na kanuni moja.

Wafundishe namna na jinsi iwapasavyo kutembea. Kwanza hukujenga ndani yako tabia. Usiwe mtu wa kanuni mbili,hali ilivyo huzuiliwa na kukosa tabia au utu wako wa ndani. (Upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu na upole kiasi.) Yote itategemea na jinsi unavyoendelea katika uongozi wako.



Namna ya kusuluhisha shida.

Kufundisha na kuonyesha kuwa kunaitwa kutafuta suluhu kunapo tokea shida katika hali yetu ya kuongozwa na kuvutia. Zingatia kusikia mawaidha ya timu yako. Ikiwa mawaidha yao ni sawa basi yakubali. Na kupitisha ya kutumika yakiwa matokeo yake ni ya muda tu basi yaonyesha jinsi ya namna ya kuleta suluhu ya kudumu.



Usimamizi.

Usimamizi ni hali ya kuchunga wakati au saa, mali,talanta, vipawa na karama zote ambazo mmoja amepewa mashirika au mataifa, chochote kile tumepewa na mungu ni chake hadi mwisho, hata pumzi tulionayo. Hivyo basi safari yetu ya maisha ina pimwa jinsi tunavyo angalia muda, mali, vipawa,talanta tulizopewa.



Uwekaji wa talanta.

Maana ufalme wa mbinguni ni kama mtu anayetaka kusafiri ng’ambo. Aliwaita watumishi wake, akawakabithi mali yake. Kila mmoja kadri na uwezo wake mmoja talanta tano, mwingine mbili na mwingine moja. Kisha akasafiri. Mara yule aliyekabithiwa tano akafanya kosa na kupata tano juu yake. Hali kadhalika na yule aliyekabithiwa mbili, lakini yule aliyekabithiwa moja akaenda akachimba shimo ardhini akaificha fedha ya bwana wake. Baada ya muda mrefu, yule bwana alirudi na kuanza kukagua kuhesabu ya matumizi na mapato ya fedha yake.



Uwajibikaji wa talanta.

Mtumishi aliyekabithiwa talanta tano akaja na faida ya zingine tano juu yake. Bwana wake akamwambia vema, mtumishi mwema na mwaminifu,”umekuwa mwanifu katika mambo madogo nitakukabithi makubwa. Njoo ufurahi pamoja na bwana wako. Aliyekabidhiwa mbili pia akaja na kumwambia bwana wake, bwana ulinikabidhi mbili tazama nimepata mbili zaidi juu yake.Bwana wake akamwambia, vema ,mtumishi mwema na mwamifu.Umekuwa mwaminifu kwa mambo madogo nitakukabithi makubwa. Njoo ufuhrahi na bwana wako.

Lakini yule aliyekabithiwa moja akasema bwana najua wewe ni mtu mgumu huna pale ambapo hukutapanya, niliogopa nikaficha fedha yako katika ardhi ,chukua basi mali yako.Bwana wake akamwambia wewe ni mtumishi mwovu na mvivu, unajua kuwa mimi huvuna mahali ambapo sikutapanya na kukusanya mahali ambapo ilikupasa kuiweka fedha yangu katika benki nami ningelichukua mtaji wangu na faida yake. Basi mnyang’anyeni hiyo fedha mkampe yule mwenye talanta kumi.

Moyo wa Yesu ambao umeongelewa katika sehemu hii ya maandiko ni juu ya usimamizi . Mambo yanayo mwelezea mtumishi mwema ni uaminifu na maradufu ya nyongesa. Hali mambo yanayomweleza mtumishi mwovu ni uvivu, uongo na kukosa kuzalisha.

“Maana aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa(Mathayo 25:14-30)

Nidhahiri kuwa mungu ni mfanyi biashara mwema. Anaangalia na kutazamia ongezeko katika uwekezaji wake kwa maisha ya kila mmoja wetu. Yoshua kwa mataifa wamejitolea kwa kuwasaidia na kufundisha watu, na mataifa kusimama wakati wao mali na talanta katika hali ya kuonyesha kimaisha.

Moja wapo ya shabaa yetu ni kuwezesha mataifa kujimudu na kujisimamia kifedha na pia kuwa wapeanaji katika mavuno makuu. Tumeenda mfano rahisi kwa bibilia ambao utaelekeza katika usimamizi wa tabia na matendo.

Fedha ambazo zimepatikana kwa kuendeleza ufalme kwa watu wenyeji eneo hilo. Hii imedhibitishwa kwa njia na mtindo rahisi utakao wezesha kila chuo kuzalisha na kuendelesha ukuwaji mwaka hadi mwaka.

Kuna mfano ulio wazi na wa ukweli. “Unaweza kumlisha mtu kwa siku samaki (Kumfanya akutegeme wewe) au mfundishe jinsi ya kuvua na ajilishe maishani mwake mwote. (kumwezesha na kumuandaa kama msimamizi wa kutunza na kuweka raslimali) Sote twakubaliana na kanuni ya mavuno ambayo kupokea mbegu, kupanda mbegu halafu kuitunza mpaka ifikie kuleta mavuno. Hata hivyo hii ndio mfano wa haki na kawaida kwa ukulima na matokeo yake. Basi kunayo kanuni iliyokuu zaidi katika hali ya uzalishaji 30,60 na 100. Ufunguo wa kuelewa hii kanuni kuu ni kuelewa kwamba kuongezeka kwa ufalme, hakupimwi na tumejikusanyia mali. Bali ni vile tumerungusha mali yetu. Jinsi mungu anaweza kutuamini kutumia wakati wetu, raslimali, vipawa na talanta kuuelekea ufalme kwa kujulisha jina lake na neno lake duniani.

Wakati wote ahadi za Mungu ni kweli na Amina hazitajulikana au kuonekana kwa wingi ikiwa tutaenda kinyume na kanuni kuongezea mbegu na mavuno. Usimamizi wema ni muhimu kwa yote tutendayo.



Download 1,15 Mb.

Do'stlaringiz bilan baham:
  1   2   3   4   5   6   7   8   9   ...   13




Ma'lumotlar bazasi mualliflik huquqi bilan himoyalangan ©hozir.org 2024
ma'muriyatiga murojaat qiling

kiriting | ro'yxatdan o'tish
    Bosh sahifa
юртда тантана
Боғда битган
Бугун юртда
Эшитганлар жилманглар
Эшитмадим деманглар
битган бодомлар
Yangiariq tumani
qitish marakazi
Raqamli texnologiyalar
ilishida muhokamadan
tasdiqqa tavsiya
tavsiya etilgan
iqtisodiyot kafedrasi
steiermarkischen landesregierung
asarlaringizni yuboring
o'zingizning asarlaringizni
Iltimos faqat
faqat o'zingizning
steierm rkischen
landesregierung fachabteilung
rkischen landesregierung
hamshira loyihasi
loyihasi mavsum
faolyatining oqibatlari
asosiy adabiyotlar
fakulteti ahborot
ahborot havfsizligi
havfsizligi kafedrasi
fanidan bo’yicha
fakulteti iqtisodiyot
boshqaruv fakulteti
chiqarishda boshqaruv
ishlab chiqarishda
iqtisodiyot fakultet
multiservis tarmoqlari
fanidan asosiy
Uzbek fanidan
mavzulari potok
asosidagi multiservis
'aliyyil a'ziym
billahil 'aliyyil
illaa billahil
quvvata illaa
falah' deganida
Kompyuter savodxonligi
bo’yicha mustaqil
'alal falah'
Hayya 'alal
'alas soloh
Hayya 'alas
mavsum boyicha


yuklab olish